HIZI NI HATUA ZA MAFANIKIO KATIKA BIASHARA YA MTANDAO.

Vipengele:

  • Ndoto (Dream)
  • Kujidhatiti (Commitment)
  • Orodha (List)
  • Kualika (Invitation)
  • Edification
  • Kuwaelimisha watu kuhusu biashara na bidhaa (Presentation)
  • Kufuatilia (Follow Up)
  • Ushauri Kutoka Kwa Aliyekutangulia kwenye biashara (Advice)
  • Duplication
  • Kuwasaidia Wengine

Ni Hatua Hizi Ndio Zitamsaidia Mwanachama Kuvunja na Kumaliza Mfumo wa Malipo

Kumekua na changamoto kubwa sana katika mfumo wa uendes-haji wa biashara hii hapa barani Afrika hususani nchini Tanzania kwani mfumo huu wa biashara umekua ukifanyika kiholela na wa-tu holela bila kutaka kujielimisha ili waweze kuifanya kwa ufasaha na kuleta manufaa kwa wahusika (wanachama), hii imepelekea kushusha hadhi ya aina hii ya biashara na kuonekana ni biashara ya ujanja ujanja na wakati mwingine wahusika kuonekana ni mat-apeli.

Ili uweze kufanikiwa katika biashara hii kuna misingi na hatua ambazo ni muhimu kuzifahamu na ukizifuata ipasavyo ni lazima ufanikiwe. Muongozo huu umeandaliwa na watu walionufaika na hatua hizo, wamekuwa wakizifuata na wamenufaika sana katika biashara hapa nchini Tanzania.

Ndoto ni msingi wa kwanza katika biashara. Unapoanza biashara kitu cha kwanza ni kujua ndoto zako au unataka nini katika maisha yako. Ndoto zako ndiyo sababu ya wewe kufanya biashara. Usipojua nini unataka kwenye biashara mwendelezo wako utakuwa hafifu kwa sababu hakuna unachokikimbiza.

Watu watajiunga na wewe wakijua kwanini unafanya hii biashara. Lakini pia hata wewe mwenyewe ukijua kwanini unafanya hii biashara? biashara yako itakuwa na maana:

  1. Ndoto zitakusaidia kukupa kusudi la kuishi duniani na unajua unataka nini?
  2. Ndoto zitakusaidia kujua ukubwa wa gharama unazotakiwa kulipa ili uweze kukamilisha malengo yako.
  3. Ndoto zitaendelea kukupa hamasa, msukumo wa kupambania au kufanya kazi kila siku (ndoto ni kama mafuta ambayo yanakupa nguvu ya kusonga mbele na kupambana).
  4. Ndoto zitakusaidia ujue unahitaji vifaa au watu wa aina gani ili uweze kukamilisha lengo lako (ndoto zitakuchagulia marafiki, aina ya mahusiano unayoingia nk. Unapoanza biashara ni vigumu sana kufanikiwa kama hauna ndoto)
  5. Ndoto zitakupa uvumilivu wa kuvishinda vikwazo na changamoto za kukatishwa tamaa, kurudishwa nyuma, kuchekwa, kudharauliwa, kuzodolewa (hivyo ndoto itakupa ngozi ngumu kama mjasiriamali)
  6. Ndoto ni kama mbawa za ndege na ndege asiyekuwa na mabawa hawezi kuruka.

ILI IWE NDOTO INABIDI IWE NA SIFA ZIFUATAZO

  1. Iandikwe kwenye daftari maalum la kudumu (Habakuki 2:1-4). Ndoto ambayo haijaandikwa hiyo siyo ndoto ni tamaa tu.
  2. Iandikwe katika wakati uliyopo. Mfano: Mimi Yusuph Mbarouk ninamshukuru Mungu na ninafuraha sana ninamiliki Helkopta.
  3. Iwe na muda wa kuikamilisha. Mfano: Mimi Yusuph Mbarouk ninamshukuru Mungu na ninafuraha sana ninamiliki Helkopta kufikia 2037.
  4. Iwe wazi na inyambuliwe nyambuliwe mpaka hatua ya mwisho. Mfano: Kama unasema nahitaji kumiliki gari. Ili hiyo ndoto iwe wazi kwako inabidi ujue ni gari ya aina gani? Ina sifa gani? Rangi gani? Ina viti vingapi? Ina cc ngapi? Inauzwa wapi? Toleo la mwaka gani? Na gharama yake ni kiasi gani.

MAMBO YA KUZINGATIA ILI UWEZE KUONGEZA KASI YA KUKAMILISHA NDOTO ZAKO.

  1. Kuwa na kitabu cha ndoto zako (vision book): hiki ni kitabu maalum ambacho umeweka picha za ndoto zako kama vile nyumba, usafiri, shule, miradi familia, maeneo ya kutembelea mfano, Mbuga ya Serengeti, Dubai nk
  2. Kuwa na picha za ndoto zako zilizobandikwa kwenye kuta za nyumba kama sebuleni, chumbani, chooni.
  3. Kuzisoma ndoto zako kwa sauti ukijisikia. Hii huongeza Imani ya kukamilisha ndoto zako kwa sababu Imani huja kwa kusikia. Ndoto utazisoma asubuhi na jioni kila siku.
  4. Kuwa na kadi yenye lengo lako kuu unalohitaji kulitimiza kwa mwaka (index card). Kadi hii unapaswa kutembea nayo kila siku, kila mahali na unaisoma.
  5. Kutembelea maeneo yenye ndoto zako na kuzishuhudia kwa macho katika uhalisia wake mfano: kutembelea showroom za magari ya ndoto yako, mtaa unaohitaji kujenga nyumba ya ndoto zako, kutembelea mitaa yenye nyumba za ndoto zako nk

ZOEZI

  1. Fikiria kama fedha siyo tatizo kabisa katika maisha yako na una mabilioni ya fedha zote ambazo ungehitaji kuzikamilisha katika maisha yako (usijiwekee ukomo) ungetamani uishi wapi? umiliki gari la aina gani? uipeleke familia yako kupumzika nchi gani? wanao wasome shule gani? umiliki gari ya aina gani? Andika ndoto 10 ambazo ungehitaji kuzikamilisha ndani ya miaka 5-10
  2. Hakikisha unatembea na kadi ya malengo yako na kuisoma mara kwa mara, hakikisha unatembea na vision book yako na unangalia picha za ndoto yako mara kwa mara. Hakikisha unaporudi nyumbani unafanya vitu vitatu: Kwanza, unavuta taswira ya ndoto zako kabla ya kulala mpaka utakapopitiwa na usingizi (Imagination), Pili, fanya tafakari wewe na Mungu usiku unapoamka kwenda haja ndogo, usirudi tu kitandani kulala (Meditation). Tatu, asubuhi unapoamka hakikisha unajitamkia maneno chanya kwenye kioo kila siku. Mfano: Mimi ni tajiri, mimi ni kichwa siyo mkia, mimi ni mshindi, mimi si maskini (Affirmation).
  3. Visualization (Maono yaliyotimia): Ni ile hali ya kuyaona malengo yako kama yametimia tayari, hakikisha unachukuwa kadi ya malengo (index card) unaenda sehemu yenye utulivu unaisoma kwa sauti mara 5-10 huku ukiyaona yale malengo yako kana kwamba yametimia tayari na kuona mambo ambayo utayafanya kama malengo yako yatatimia. Hii ni tafakari ya ndani kabisa katika akili yako. Ukirudi nyumbani kwako hakikisha unaangalia picha za malengo yako katika hali ya utulivu.

Kaa chini ujue katika wiki yako siku gani unafanya biashara? (siku zako ambazo unafanya biashara inabidi uzijue na siku ambazo hufanyi biashara inabidi uzijue) pia taja muda ambao unafanya biashara katika siku husika.ujitoa ni msingi namba mbili katika biashara hii ya BF Suma. Mafanikio katika biashara hii yanakutegemea wewe mwenyewe. Wewe ndiye unayewajibika kwa matokeo chanya au hasi katika biashara hii.Mtu aliyekuunganisha katika biashara hii kazi yake kubwa ni kukufanya ujitegemee. Kazi yake siyo kukufanyia wewe kazi. Kazi yake ni kukusaidia uweze kujisimamia utimize malengo yako na uweze kusaidia wengine kujisimamia kwenye timu yako.Ukubwa wa ndoto ulizonazo utakusaidia uweze kujitoa muda gani? Katika biashara yako. Kumbuka umeanza biashara hii na siyo biashara ya kiongozi wako (upliner) bali hii ni biashara yako “Kupata vitu ambavyo hujawahi kuvipata ni lazima ufanye vitu ambavyo hujawahi kuvifanya” ukijitoa Zaidi utapata Zaidi, ukijitoa kidogo utapata kidogo. Kuwa na ndoto ni swala moja na kutimia kwa ndoto zako kunategemea kujitoa kwako.Katika hii biashara unafanya kwa masaa yote au kwa muda wa ziada (full or part time) kama uko katika biashara masaa yote (full time) kazi gani umepanga kuzifanya ndani ya siku nzima? Kama uko part time utafanya kazi za BF Suma saa ngapi hadi saa ngapi? Katika masaa yako ya ziada?

Unatumiaje weekend zako? Uko tayari kuwekeza katika biashara zako? Vitu gani uko tayari kuviacha ambavyo havikusaidii na vinakula muda wako kukamilisha ndoto zako? Mfano: kuwangalia mpira, kuwangalia movies, kupoteza muda kwenye mitandao ya kijamii whatsapp, facebook, instragram, youtube channel ambavyo vinakupotezea muda.

Uko tayari kuwekeza fedha kwa ajili ya kulipia matangazo kwenye mitandao ya kijamii, kulipia mikutano, kutumia bidhaa wewe mwenyewe, kutoa sample kama kahawa, coll roll, kununua vitabu nk.

Uko tayari kujitoa miezi 18 mfululizo kujenga biashara yako na mtazamo wa kufanikiwa (soma hatua 5 za mafanikio ya BF Suma). Unapoanza biashara hii unakuwa hujui vitu vingi kama vile: kuwalika watu, hujui kuongea na watu, hujui kuelimisha watu biashara au bidhaa, hivyo hupati matokeo na wengi huishia njiani badala ya kujifunza ili wajue kufanya vitu kwa usahihi na wapate matokeo chanya. Jipe muda wa kufanya vitu sahihi na matokeo yatakufuata.

Miezi 18 ni miezi ya kujielimisha, kujijenga na kuweza kuwa mahili katika mbinu zote za biashara. Ili ufanikiwe epuka mhaho wa biashara ya mtandao (panic) kuhaha pale ambapo hupati matokeo ya haraka katika biashara ya mtandao jipe miezi 18.

ZOEZI

1. Uko tayari kuwekeza shilingi ngapi katika biashara yako ili isonge mbele kwa kuwekeza katika biashara yako, kununua bidhaa za sample wakati wa semina zako?

2. Uko tayari kuwekeza katika vifaa vyako vya biashara kama diary, notebook ya orodha, kununua vipeperushi, kuprint picha za ndoto zako, kununua vitabu, kununua script za kupiga simu, kununua bidhaa wewe mwenyewe.

3. Je, uko tayari kuwekeza kiasi gani cha fedha
Kufanya au kujitamkia maneno chanya katika maisha yako kila siku (Affirmation).

Baada ya kujisajili katika mfumo huu wa biashara, una wajibu wa kuandaa orodha ya majina ya watu ambao watakuwa watarajiwa wateja au watu ambao utafanya nao kazi pamoja (TEAM YAKO)

Ili upate watu, inabidi uandae orodha ya majina ya watu wenye sifa zifuatazo kama ilivyoainishwa kwenye jedwari hapa chini ambao utaanza kuwapigia simu ili wawe wateja au Team yako.

Kuna tabia kuu 4 za watu ambazo unapaswa kuzijua kama ifuatavyo (Tumia chati ifuatayo);-

S/NO JINA SIMU ANA FUNDISHIKA ANA USHAWISHI ANA MTAJI ANAJITEGEMEA KIMAWAZO

 

1.
2.
3.
4.
5.
6.
  1. ANA FUNDISHIKA

Ni mtu ambaye anasikiliza na kujifunza vitu vipya na kuvifanyia kazi.

  1. ANA USHAWISHI

Ni mtu ambaye mawazo yake yanaheshimika na watu wengi kama vile Mwanasiasa, Mchungaji, Sheikh, Msanii, Mbunge, Mwalimu, Rais wa chuo, Kiongozi wa chama, amefanikiwa kiuchumi, Mwalimu wa kwaya, MC (hawa ni aina ya watu ambao wakiongea watu wana wasikiliza na kuwafuata)

  1. ANA MTAJI

Ni mtu ambaye akishirikishwa biashara na akailewa anaweza kujiunga maana ana mtaji wa kujiunga katika biashara. Mtaji siyo kikwazo kwake, huyu anaingiza kipato na anaweza kujiunga na kifurushi chochote.

  1. ANAJITEGEMEA KIMAWAZO

Ni mtu ambaye anajiamini na kama akielewa biashara yuko tayari kufanya na atakupeleka kwa watu wengine haraka sana, anaye elimisha watu wengine bila kumtegemea kiongozi wake (upliner)

Kwenye kila jina la mtu uliyemuandika kwenye kila tabia kama mtu huyo anatabia hiyo weka tiki (Ö)  na kama hana tabia hiyo weka (x)

Hii itakusaidia kuanza na watu sahihi zaidi. Watu ambao wana ushawishi, fundishika, wana mtaji, na wanajitegemea kimawazo. Unapochagua mtu wa kumuelimisha biashara anza na yule mwenye tiki 4 na ana tabia zote 4 ambazo ni ushawishi, fundishika, wana mtaji, na wanajitegemea kimawazo.

Baada ya kuandaa orodha yako na kuweka tiki (Ö) kwenye tabia zote 4 walizonazo watu wako. Kitu kinachofuata ni kufanya presentation kama ifuatavyo:- Anza kufanya presentation kwa watu wenye tiki 4 kisha wenye tiki 3, wenye tiki 2, wenye tiki 1 na kisha maliza na wasio na tiki kabisa.

ZINGATIA

Unapoanza biashara watu wenye tiki 4 unawafanyia presentation kwa msaada wa kiongozi wako (upliner). Watu wenye tiki 4 watajiunga kwenye biashara maana wanafundishika, wanaushawishi, wanamtaji, wanajitegemea kimawazo na kivitendo na hawa watafanya biashara yako iende kwa speed kubwa na kuleta matokeo makubwa na kukupa watu wenye tabia kama zao.

Watu wenye tiki 3, 2, 1 au hawana tiki kabisa wafanyiwe presentation na downliners wa upliner wako.

AINA ZA WATU KWENYE BIASHARA YA MTANDAO

  1. Wababaishaji namba 1

Hawa ni watu ambao wana watu wao kichwani mwao ambao ni majembe yao. Kwa hiyo kufanikiwa kwa watu kunategemea maamuzi ya hao watu, wakikubali biashara inakuwa nzuri kwao. Wakiikataa wanaona biashara hii ni mbaya na haifai. Hawa ni watu ambao wanawafanyia maamuzi watu wengine ambao hawaja wafanyia presentation kwao mtu hu-join au kut-join katika biashara kwenye akili zao kwanza wanaongoza kuwaamulia watu kabla ya kuwaambia biashara (hawa ni watu ambao hawana madaftari maana watu wao wako kichwani)

  1. Mbabaishaji namba 2

Huyu ni mtu ambaye anaandika watu 100-150 maana ana hofu yake kubwa ni kuishiwa watu. Anapowapigia simu watu presha inapanda na presha inashuka ya kuishiwa watu maana hana plan ya kuongeza watu wapya kwenye orodha yake.

  1. Mtaalamu:

Huyu anaandika orodha kubwa, anatoa watu kwenye simu na kuwaandika kwenye daftari na anakuza orodha yake kwa kuongeza watu 2 kila siku maana anaamini watu ni kama mchanga wa bahari na hawaishi. Hawafanyii watu maamuzi na anajua kanuni ifuatayo “anza kuchimba kisima kabla hujasikia kiu”

NAMNA YA KUWAALIKA WATU ILI WAJE KUJIFUNZA BIASHARA AU KUWAELIMISHA JUU YA BIDHAA.

NAMBA 1

JINSI YA KUWAPIGIA SIMU KUWAALIKA WATU KUJA KWENYE SEMINA AU KUWAELIMISHA

  • Kuwaalika mteja wako ni moja ya stadi muhimu sana ili waweze kufanikiwa sana kwenye biashara yako
  • HAKIKISHA UNA ORODHA YA WATU 250 unaotaka kuwafikishia ujumbe wa BF SUMA
  • Usiwe na papara, fuata utaratibu wa kupiga simu na watu wako watakuelewa tu
  • Ni kawaida kwa mtu unapoanza kukosea hapa na pale ila ukirudia mara kadhaa utakuwa vizuri, kila mmoja alianza akiwa hajui ila kwa kurudia rudia akawa anajua, UTAWEZA
  • Lengo la kuwalika/KUPIGA SIMU NI KUMPA MTU HAMASA (CURIOSITY)
  • MTU WAKO ANAPOKUJA /UNAPOONANA NAE TUMIA VIFAA/VYENZO/TOOLS KUMUELIMISHA KUHUSU BF SUMA, USIMWELEZE KWENYE SIMU HATAELEWA KABISA. VIFAA/VYENZO/TOOLS NI KAMA MAGAZINE, VIDEO ZA FURSA. Tembelea Website ya Kiswahili ya www.dreamteamtz.com, VIDEO ZA USHUHUDA, MAGAZINE SOFT COPY
  • MTU ANAPOKUWA NJE YA MKOA TUMIA VIDEO/MTUMIE MAGAZINE KWA WHATSAPP

Lengo si kumweleza na kumuelimisha kuhusu BF SUMA kwenye simu, ukifanya hivyo mambo yafuatayo yatakutokea: Utatumia nguvu kubwa sana na vocha nyingi kumueleza hadi aelewe na kama akikuelewa atakuambia yeye hawezi kuwaeleza watu wengine kama wewe hadi ajifunze kwanza

MASWALI AMBAYO UTAULIZWA NA WATU UNAPOWAPIGIA SIMU NA NAMNA SAHIHI  YA KUJIBU

SWALI 1: Ni biashara gani? Au si uniambie tu kwenye simu?

JIBU: KUNA VITU VYA KUONA NA KUJIELIMISHA, NIKIKUELEKEZA KWENYE SIMU HATA HUWEZI KUNIELEWA, VILEVILE BIASHARA HII INAWEZA IKAKUFAA AU ISIKUFAE, NINAPENDA TUONANE, NIKUONYESHE PICHA KUBWA ILI UFANYE MAAMUZI SAHIHI. MUDA WAKO UKOJE ILI TUWEZE KUONANA.

SWALI 2: Hii ni biashara kama ya Forever au Aim Global Au Ole frem?

SIYO KILA MTU ANAYEKUULIZA SWALI HILI ANA MTAZAMO HASI JUU BIASHARA YA MTANDAO. HAKIKISHA UNAJUA KWANINI ANAKUULIZA SWALI HILO ACHA KUJITETEA NA KUHISI AMEKUULIZA HIVYO KWA SABABU YUKO HASI.

JIBU: NDIO, MUULIZE UMEWAHI KUFANYA BIASHARA YA AINA HII AU UNAMFAHAMU MTU ALIYEWAHI KUFANYA BIASHARA KAMA HII? MSIKILIZE  ILI UJUE KWANINI AMEKUULIZA SWALI HILI? AKUAMBIE CHANGAMOTO ALIZOPATA HALAFU JIBU: UKIONA BIASHARA ISIYO NA CHANGAMOTO HIZO BADO UPO TAYARI KUJIELIMISHA? MSIKILIZE…MUULIZE, SIKU IPI NI NZURI TUONANE  ILI NIKUELIMISHE?

NAMBA 2

UFUATAO NI UTARATIBU RAHISI WA KUMUALIKA MTU

  1. JIAMINI: Unayeongea nae hajui kama unakosea au unapatia
  2. MTAJE KWA JINA: Helloo Shukran
  3. MUULIZE KAMA YUPO SEHEMU NZURI UONGEE NAYE: Una dakika moja ya haraka tuongee?
  4. MSIFIE: Nimekupigia simu hii kwa sababu wewe ni muelewa sana
  5. ONYESHA THAMANI KWA KUMUULIZA: KWA MFANO. UKIONA BIASHARA INAYOWEZA KUKUONGEZEA KIPATO CHA ZIADA BILA KUATHIRI SHUGHURI ZAKO NA KWA MTAJI MDOGO, UNAWEZA KUJIELIMISHA UONE KAMA ITAKUFAA?
  6. ONYESHA KAMA HUMUHITAJI: KUNA BIASHARA NIMEIANZA AMBAYO INAWEZA KUINIONGEZEA 100,000 HADI 500,000 KWA WIKI NA KWA MTAJI MDOGO SANA, INAWEZA IKAKUFAA AU ISIKUFAE. IKIKUFAA NI VYEMA NA ISIPOKUFAA NI VYEMA PIA.
  7. CHAGUA NJIA SAHIHI YA KUMUELIMISHA, UNAYOPENDA: KWA SABABU KUNA VITU VYA KUONA, KUJIELIMISHA NA KUONJA. MFANO NIKUKUALIKA KWENYE SEMINA KESHO SAA 8 MCHANA HAPA KIMARA STOPOVER, SHANGO HOUSE GOROFA 1, UNAWEZA KUJA NIKUELIMISHE UONE KAMA NI KITU KINACHOKUFAA?

KAMA YUKO NJE YA MKOA

KABLA HUJATUMA VIDEO HAKIKISHA MTU ANA DK 45 HADI LISAA 1 LA UTULIVU. UNAPOPIGA SIMU LENGO LAKO NI KUPATA MIADI YA YEYE KUANGALI VIDEO SIYO KUMTUMIA VIDEO.

Kwa mfano nikukutumia Link ya video fupi kwa whatsapp inayoelezea kila kitu unaweza kuiangalia uone kama itakufaa? (unaweza kumtumia link akaangalia moja kwa moja Youtube au unaweza kumwambia apakue telegram ili umtumie kupitia telegram aangalie video nzima)

KAMA UNATAKA KUONANA NAE UNASEMA:

Muda wako ukoje twaweza kuonana nikuelezee kila kitu, kawaida ninaonana na watu ofisini kwangu KIMARA STOPOVER, SHANGO HOUSE GOROFA 1 kila siku saa 8 mchana hadi saa 11 jioni. Je, huu ni muda mzuri kwako?

NAMBA 3

JINSI YA KUWALIKA RAFIKI ZAKO NA NDUGU UNAOELEWANA NAO SANA/ ULIONAO KARIBU

(NJIA YA KIBABE)

Helloo Shukran una dakika moja ya haraka tuongee?

Siku ya alhamisi una kitu gani ambacho unakifanya kinachoweza kukuingizia 500,000 kwa wiki?

Hakuna

Ninakuwalika siku hiyo kwenye semina itakayoweza kukuingizia 500,000 KWA WIKI KWA KUTUMIA MUDA WAKO ZIADA NA KWA MTAJI MDOGO. KUTAKUWA NA WAJASIRIAMALI WALIOFANIKIWA

NI BIASHARA GANI HIYO?

Kuna vitu vya kuona na kujielimisha, nikikuambia kwenye simu hata huwezi kunielewa. Ukija kwenye semina utapata picha kubwa.

Kwa hiyo utakuwepo alhamisi saa 8 ili nikuwekee nafasi?

NAMBA 4

JINSI YA KUWALIKA WATU WALIOKUZIDI KIUCHUMI, WENYE USHAWISHI MKUBWA AU WALIOFANIKIWA SANA

MFANO: WACHUNGAJI, WABUNGE, MA CEO, MATAJIRI NK

Lengo la kumpigia simu mtu huyu ni ili upate wasaa wa kukutana naye umuelimishe bidhaa zetu na mfumo wa malipo ili ajiunge au anunue bidhaa au akukutanishe na watu ambao wanaumwa ili wawe wateja wako au akukutanishe na watu watakaojiunga kwenye biashara yako

KUMBUKA: MTU HUYU UNAWEZA KUONANA NAYE HUKO ALIKO

NAMNA YA KUMPIGIA SIMU

HELLOO (MSALIMIE KUTOKANA NA NAFASI ALIYONAYO)

HELLOO!! BABA MCHUNGAJI SHIKAMOO. UNA DAKIKA  MOJA YA HARAKA TUONGEE KUNA KITU CHA MUHIMU SANA NINATAKA UNISAIDIE. KUNA BIASHARA NIMEIANZA. KWA SABABU WEWE UNAKUTANA NA WATU WENGI NA UMEONA VITU VINGI KULIKO MIMI. NILIKUWA NINAOMBA UNISAIDIE KUNISHAURI NA KUNIKUTANISHA NA WATU AMBAO NITAWAHUDUMIA NA KUWASAIDIA KUPITIA BIASHARA HII. SASA KWA SABABU KUNA VITU VYA KUONA, KUJIELIMISHA NA KUONJA NIKIKUELEZEA KWENYE SIMU HATA HUWEZI KUELEWA. NINAOMBA NIPATE WASAA NA WEWE WALAU DK 30 ENEO AMBALO LITAKUWA CONFOTABLE KWAKO ILI NIWEZE KUKUONYESHA, KUKUONJESHA NA KUKUELIMISHA, SIKU GANI ITAKUWA NI NZURI KWAKO ILI TUONANE.

AKICHAGUA MUDA MWAMBIE NITAKUJA NA BUSINESS PARTNER WANGU ILI UTUSHAURI KWA PAMOJA.

NAMBA 5

NAMNA YA KUPATA WATU ZAIDI

KILA UNAEMUELIMISHA BF SUMA ANA NAFASI YA KUKUPA WATEJA (WAGONJWA ANAOWAFAHAMU) NA WATU WATAKAO JIUNGA KAMA UKIJUA NAMNA YA KUMUOMBA

JINSI YA KUPATA WATEJA ANA WATU WENGI ZAIDI KUTOKA KWA KILA MTU UNAE MFANYIA SEMINA NA JINSI YA KUWAPIGIA SIMU WATU HAO ULIOPEWA NA KUWAALIKA KWENYE SEMINA AU KUWAELIMISHA

  • Je, unajua kila mtu unayemfanyia semina BF SUMA ana watu nyuma yake? Mtu mmoja anaweza kukutanisha na watu wengine wengi ambao watakuwa wateja wako wakubwa wa bidhaa au watakaojiunga kwenye biashara.
  • Skills hii ya kuwatumia unaowafanyia semina au wateja wako kukuunganisha na watu wengine itakusaidia kupata watu wengine wapya kila siku wa kuwauzia bidhaa na kuwafundisha biashara.
  • Unapomfanyia semina mtu mmoja nyuma yake ona kuna watu zaidi ya 250
  • KAMWE USIWE KAMA WATU WENGINE ambao wanapofanya semina kwa watu wanamuacha anaondoka hivi hivi bila ya kuchukuwa watu wake ambao anapenda kujiongezea kipato cha ziada au wenye matatizo ya kiafya ambao bidhaa zitawasaidia.
  • KUMBUKA: Mtu unayemfanyia semina ni daraja la kukutanisha na watu wengine wenye matatizo ya kiafya na wanaopenda kujiongezea kipato hivyo leo nakufundisha jinsi mtu huyo atakavyokupa watu wengine watakao kuwa wateja wako na watakaojiunga na wewe

BAADA YA KUFANYA SEMINA KWA MTU/WATU

Hakikisha amekupa namba na amekutambulisha kwa watu wake anaodhani wanapenda pia kujifunza zaidi juu ya biashara inayoweza kuwaongezea kipato cha ziada na bila kuwathiri shughuli zao

Pia hakikisha amekupa tena namaba za watu ambao anadhani wakipata ELIMU juu ya bidhaa za BF SUMA watatua changamoto zao za KiafyaANAKUPAJE NAMBA ZA WATU ANAOWAJUA WENYE CHANGAMOTO ZA KIAFYA NA WANAOTAKA KUJIONGEZEA KIPATO?

NI RAHISI SANA: Mtumie jumbe zote mbili kwenye simu yake UJUMBE WA AFYA NA UJUMBE WA BIASHARA (JUMBE ZINAJIELEZA ZENYEWE) Mwambie AWATUMIE WATU WAKE HALAFU AKUPE MAJINA NA NAMBA ZAO, kwa yeye kuwatumia ujumbe anakuwa amekutambulisha katika bidhaa zako utakazoanzia na utaongeza fedha kidogo iliyobaki kukamilisha fedha ya kuwanzia na hongera umepata mteja wa kuwanza nae

JINSI YA KUJIBU CHANGAMOTO KATIKA ZOEZI LA KUCHUKUWA NAMBA ZA WATEJA NA NAMBA ZA WATU WAKE WATAKAOFANYA BIASHARA

  1. HADI NIONGEE NAO KWANZA NDIO NIKUPATIE NAMBA

JIBU: Mimi nina uzoefu na ninazijua bidhaa vyema na ninajua kuelezea vizuri zaidi yako, wewe ukiulizwa maswali mawili tu hutoweza kujibu na mtu atakuona hujui hivyo hatofanya maamuzi mazuri, hivyo mimi ninajua zaidi nitakusaidia kuongea nao na ujumbe niliokutumia ukiwatumia wataelewa huna haja ya wewe kuongea sana.

  1. NIKIENDA NYUMBANI NITAKUTUMIA MAJINA USIWE NA HOFU HII SIMU YANGU HAINA WATU HADI NICHUKUE SIMU KUBWA HALAFU NATAKA NICHAGUE WATU

JIBU: Nakuelewa sana ila nimeongea na watu wengi sana wanapotoka hapa mambo yanakuwa mengi sana, na mimi ninakuwa na watu wengi sana, najua utakuwa nao wachache hapo ulipo unaowakumbuka tuanze na hao. Lengo ni kuwaelimisha kama nilivyokuelimisha, nao wataamua wenyewe.

  1. SASA IKITOKEA WATU WANGU WAKANUNUA KABLA MIMI SIJAJIUNGA AU WAKAANZA KABLA MIMI SIJAANZA

JIBU: Mtu anapoanza maana ataanza na timu sasa na unapoanza na timu maana yake mwisho wa mwezi utapata fedha/hivyo hivyo itakusukuma kupata fedha haraka ya kuanza kwa sababu unajua lazima mwisho wa mwezi utapata fedha, na kama mtu wako akinunua maana yake umepunguza gharama ya kujiunga maana yake mtu wako aliyenunua bidhaa zake tutazijumlisha kwako.

UJUMBE WA BIASHARA KWA AJILI YA WATU WAKE WANAOPENDA KUJIONGEZEA KIPATO (FURSA)

Habari natumaini ni kwema? Kuna Rafiki yangu anaitwa (weka jina lako na namba yako MFANO: YUSUPH – +255 718 172 170) Amenielimisha biashara ambayo inaweza kuniingizia kipato cha ziada cha 100,000 hadi 500,000 kwa wiki bila kuathiri shughuli zangu kwa mtaji mdogo sana nimemwomba akupigie naomba umsikilize, akuwalike kwenye semina ukae nae uone kama itakujaa. AHSANTE (WEKA JINA LAKE LINALOJULIKANA NA NAMBA YAKE) MFANO SHUKRAN 0676 114316)

UJUMBE KWA WATU WENYE CHANGAMOTO ZA KIAFYA AMBAO BIDHAA ZA BF SUMA ZITAWASAIDIA, HAWA WATAKUWA NI WATEJA WAKE WA KWANZA AMBAO UMEMSAIDIA KUONGEA NAO

Habari natumaini ni kwema? Kuna rafiki yangu anaitwa (WEKA JINA LAKO NA NAMBA YAKO YA SIMU, MFANO: YUSUPH +255 718 172 170) Amenishirikisha dawa nzuri za Kiafya kutoka MAREKANI ambazo zimewasaidia watu wengi sana wenye changamoto za Kiafya, nimemuomba akupigie simu akuelimishe, naomba umsikilize naamini hizo dawa zitakusaidia sana. AHSANTE (WEKA JINA LAKE LINALOJULIKANA NA NAMBA YAKE)

NAMBA 6

JINSI YA KUWAPIGIA SIMU WATU HAO ULIOPEWA NA KUWAALIKA KWENYE SEMINA AU KUWAELIMISHA

HAKIKISHA AMETUMIWA UJUMBE WA KUKUTAMBULISHA

HATUA

  1. JIAMINI
  2. MTAJE KWA JINA: Hello Shukran
  3. JITAMBULISHE: Unaongea na Mbarouk namba yako amenipa Shukran bila shaka unamfahamu na bila shaka alikutumia ujumbe kuwa Mbarouk atakupigia.
  4. MSIFIE: Shukran aliniambia wewe ni mtu wake wa karibu na mwelewa sana
  5. ONYESHA THAMANI: vilevile aliniambia kwamba kama ukiona biashara inayoweza kukuongeza kipato cha ziada bila kuwathiri shughuli zako na kwa mtaji mdogo unaweza kujielimisha uone kama itakufaa
  6. ONYESHA KAMA HUMUHITAJI: Nilimuelimisha Shukran biashara inayoweza kuniingizia 100,000 hadi 500,000 kila wiki kwa mtaji mdogo akawa ameipenda sana na akaomba nikupigie nawe pia nikuelimishe huenda itakufaa au isikufae ila kwa sababu kuna vitu vya kuona na kujielimisha, mfano nikikuwalika ofisini kwangu hapa KIMARA STOP OVER, SHANGO HOUSE GOROFA YA 1 leo saa 8 mchana unaweza kuja kujielimisha uone kama itakufaa au laa?

KAMA YUKO MBALI NA HAWEZI KUJA TUMIA WHATSAPP VIDEO, SEMA

Nilimuelimisha Shukran biashara inayoweza kuningizia 100,000 hadi 1,000,000 kila wiki kwa mtaji mdogo akawa ameipenda sana na akaomba nikupigie nawe pia nikuelimishe huenda itakufaa au isikufae, ila kwa sababu kuna vitu vya kujielimisha mfano nikikutumia video fupi ya whatsapp unaweza kuangalia uone kama itakufaa au laa?

AU KAMA UNATAKA AJE KWENYE SEMINA, SEMA…

Nilimuelimisha Shukran biashara inayoweza kuningizia 100,000 hadi 1,000,000 kila wiki kwa mtaji mdogo akawa ameipenda sana na akaomba nikupigie nawe pia nikuelimishe mfano nikikuwalika kwenye semina leo saa 8 mchana unaweza kuja kujielimisha uone kama itakufaa?

NAMBA 7

NAMNA YA KUKUZA ORODHA YAKO NA KUPATA WATU WA KUWAAMBIA BIASHARA YAKO KILA UNAPOKUWA

Kila mahali kuna watu, popote ulipo unaweza kupata mtu atakayekuwa kiongozi mkubwa BF SUMA, usimdharau mtu usiyemjua, kila unayekutana naye ni dhahabu, unaweza kukutana na mtu mahali popote au hata kwenye mitandao ya kijamii kama vile facebook, instragram nk

Unapoonana na mtu barabarani, kanisani, msikitini, shuleni, dukani, chuoni, kwenye daladala au kwenye kituo cha mabasi tabasamu, anzisha mazungumzo yeyote muulize vitu vya kawaida, anafanya kazi gani? mwenyeji wa mkoa gani?  Ana muda mrefu anaishi Dar es salaam? usione aibu kujieleza kidogo pia muulize maswali haya hapa chini ili kumpeleka kwenye biashara.

MASWALI YA MOJA KWA MOJA

  1. Nje na kazi yako una biashara yeyote unayofanya inayoweza kukuingizia kipato kwa muda wako wa ziada? MSIKILIZE JIBU LAKE AKIMALIZA ENDELEA KWA KUSEMA

 

Nimepatner na kampuni ya Kimarekani inayoitwa Bright Future sasa tunaongeza wigo wa soko hapa Dar es salaam hivyo tunatafuta watu waelewa ambao wapo chanya na wanaotafuta kujiongezea kipato kwa kutumia muda wao wa ziada kwa sababu kuna vitu vya kuona na kujielimisha namba yako ipi nzuri ili niweze kukualika kwenye semina zetu na kukutumia taarifa zaidi uone nini tunafanya na namna unavyoweza kutumia muda wako wa ziada kwa mtaji kidogo kuanzisha biashara kubwa na sisi?

 

  1. Ulisha wahi kufikiria kujiongezea kipato kwa kufanya biashara katika muda wako wa ziada? MSIKILIZE JIBU LAKE AKIMALIZA ENDELEA KWA KUSEMA

 

Nimepatner na kampuni ya Kimarekani inayoitwa Bright Future sasatunaongeza wigo wa soko hapa Dar es salaam hivyo tunatafuta watu waelewa ambao wapo chanya na wanaotafuta kujiongezea kipato kwa kutumia muda wao wa ziada kwa sababu kuna vitu vya kuona na kujielimisha namba yako ipi nzuri ili niweze kukualika kwenye semina zetu na kukutumia taarifa zaidi uone nini tunafanya na namna unavyoweza kutumia muda wako wa ziada kwa mtaji kidogo kuanzisha biashara kubwa na sisi?

 

  1. Kwa mfano ukiona biashara ambayo inaweza kukuongezea kipato bila kuathiri shughuli zako na kwa mtaji mdogo unaweza kujielimisha uone kama itakakufaa? MSIKILIZE JIBU LAKE AKIMALIZA ENDELEA KWA KUSEMA

 

Nimepatner na kampuni ya Kimarekani inayoitwa Bright Future sasa tunaongeza wigo wa soko hapa Dar es salaam hivyo tunatafuta watu waelewa ambao wapo chanya na wanaotafuta kujiongezea kipato kwa kutumia muda wao wa ziada kwa sababu kuna vitu vya kuona na kujielimisha namba yako ipi nzuri ili niweze kukualika kwenye semina zetu na kukutumia taarifa zaidi uone nini tunafanya na namna unavyoweza kutumia muda wako wa ziada kwa mtaji kidogo kuanzisha biashara kubwa na sisi?

 

MASWALI YA KUPITIA MLANGO WA NYUMA (YASIYO YA MOJA KWA MOJA)

Nimepatner na kampuni ya Kimarekani inayoitwa Bright Future sasatunaongeza wigo wa soko hapa Dar es salaam hivyo tunatafuta watu waelewa ambao wapo chanya na wanaotafuta kujiongezea kipato kwa kutumia muda wao wa ziada mfano, unamfahamu mtu yeyote hapa Dar es salaam aliye chanya, anayependa kujiongezea kipato cha ziada bila kuwathiri shughuri zake?

SWALI LA LAZIMA LITAKALOKUFANYA UCHUKUE NAMBA YAKE NA AJUE LENGO LAKO KUBWA NI NINI UKIWA NA NAMBA YAKE (SWALI LA KUMALIZIA)

Kwa sababu kuna vitu vya kuona na kujielimisha, namba yako ipi nzuri ili niweze kukualika kwenye semina zetu au kukutumia taarifa zaidi uone nini tunafanya na namna unavyoweza kutumia muda wako wa ziada na mtaji kidogo kuanzisha biashara kubwa na sisi?

NOTE: Uliza maswali hayo ukiwa unachati na watu/mtu WhatsApp, facebook, instragram, kwenye daladala yatakusaidia kukuza orodha yako. Hii ni mission ya kila siku ambayo unapaswa kuifocus ili ikusaidie kukuza orodha yako.

Ni kitendo cha kumnyanyua au kumuongelea vizuri mtu au kifaa ambacho kitatumika kumuelimisha mtu wako biashara. Kati ya wewe na mteja wako kuna uaminifu yaani mtu unayefahamiana naye, anakuamini ila hakuheshimu.

Kati ya mtu wako na kiongozi au kifaa kuna heshima watu wanatabia ya kumheshimu mtu wasiyemjua kama utamheshimisha kwao kwa kumnyanyua au kumuongelea vizuri

Edification unafanya kwa ajili ya biashara siyo kwa ajili ya kiongozi wako. Mtu yeyote aliyeanza biashara kabla ya wewe anavitu anavifahamu ambavyo wewe huvifahamu hivyo mtumie aweze kukuelimishia mtu wako ila hakikisha unamheshimisha/mnyanyua kabla hujamtumia kufanya kazi yako hiyo ndiyo maana halisi ya edification.

NAMNA YA KUFANYA EDIFICATION

Unapofanya edification kuna maeneo manne ambayo ni lazima ugusie:-

  1. Taarifa
  2. Fedha
  3. Safari na vitu vya kufurahisha
  4. Support

Hayo ni maeneo ambayo watu huvutiwa nayo kutokana na jinsi walivyo. Kuna watu wanaovutiwa na mtu anayezijua taarifa zote za kampuni ya BF Suma kwa hiyo unapomfanyia edification kiongozi hakikisha unasema anataarifa zote juu ya kampuni ya BF Suma.

Kuna watu wanavutiwa na fedha na ushindani au kushinda hivyo unavyomfanyia edification kiongozi hakikisha umesema amejipostion katika nafasi nzuri ya kuingiza fedha nyingi katika Bf Suma na kama ameshinda safari sema, kama ameshinda gari sema. Kama hana gari wala hajashinda safari sema amejipostion katika nafasi nzuri ya kuingiza fedha nyingi.

Kuna watu wanavutiwa furaha/vibeeeeee kwa hiyo unapomfanyia edification kiongozi sema utafurahia ukiongea naye.

Kuna watu wanavutiwa na support kwa hiyo unapomfanyia edification sema amewasaidia watu wengi sana kuweza kujiongezea kipato/.

Kwa kufanya hivyo utakuwa umegusa makundi yote ya watu hivyo kuongeza heshima kwa kiongozi wako.

Kwa hiyo heshima + Imani = mafanikio

Kumbuka baada ya kumfanyia edifiacation kaa kimya.

Mfano wa kumfanyia edification kiongozi: Yohana naomba nikukutanishe na Nelson ambaye amejipostion katika nafasi nzuri ya kuingiza fedha nyingi, utamfurahia ukiongea naye na amewasaidia watu wengi kuweza kujiongezea kipato.

Unapowapigia simu watu lengo kubwa siyo kuwaambia biashara bali kuwatengenezea hamasa ya kutaka kujua biashara Zaidi. Pia unapompigia mtu simu uwe unajua unataka kutumia njia gani kumuelimisha juu ya biashara.

Kuna njia nyingi za kumuelimisha mtu biashara:-

  1. Kutumia magazine (Bright Future Magazine) unapokutana na mtu wako
  2. Kwa kutumia video zilizoko kwenye flash utakayoichomeka kwenye TV ya nyumbani kwako au nyumbani kwa mtu wako (Home part). Flashi ina video zinazoelezea biashara, shuhuda za watu waliopona, watu waliosafiri na washindi magari.
  3. Semina za Super Sonic Speed ambapo mgeni wako anakutana na wanachama wengine na anapata shuhuda za watu waliofanikiwa hivyo semina kitu cha kwanza kuzingatia kwenye kila vifaa epuka kuwa mjumbe hakikisha unakuwa na ujumbe. Usipotumia vifaa kama vile magazine, video ya biashara, flash, semina za ukumbini, mambo yafuatayo yatatokea.
  • Utatatumia nguvu kubwa sana na mtu wako hataelewa au ataelewa ila akihisi ninabidi akariri kama wewe. Zingatia mwelimishe mtu biashara kwa njia rahisi kiasi ambacho na yeye ataona ni rahisi kufanya presentation (Dublicaton)
  1. Kwa mtu aliye mbali unatumia video ya biashara inayolipa.

Zingatia unapotaka au unapomwalika mtu atazame video ya biashara tumia script/maneno kama yalivyo andikwa katika ukurasa… vitu vya kuzingatia unapomuelimisha mtu biashara:

  1. One on one
  • Hakikisha una Bright Future Magazine
  • Hakikisha una fomu ya ushindi (fomu ya kujaza mtu anapoanza Biashara)
  • Kama unasmart phone hakikisha una shuhuda za bidhaa utakazo msikilizisha unapo muelimisha kuhusu bidhaa, pia shuhuda za watu walioshinda safari na magari.
  1. Semina za ukumbini: Uwe na magazine, utakayoitumia baada ya semina kumuelisha mtu wako na kumuonesha shuhuda. Lazima uwe ukumbini. Hii itakusaidia kujifunza, kuelimisha kupitia kwa kiongozi wako anavyofanya pia kufuatilia na kuelewa semina. Uwe mjumbe wa kuwatumia watu wako. Lazima uwe na diary, fomu ya ushindi kulingana na idadi ya watu wako.
  2. Link za video: hii ni kwa mtu aliyembali. Kama unamtumia mtu aliyembali hakikisha mtu huyo ana muda angalau dk 45 za kuangalia video. Hakikisha mazingira rafiki na hawezi kuingiliwa na kitu chochote anapoangalia video, ikiwa hayupo katika mazingira rafiki na hana dk 45 hakikisha una panga nae muda rafiki wad k 45 na akiwa katika mazingira rafiki ya kuangalia video. Heshimu njia hii ya kumuelimisha mtu kama njia nyingine. Mtu asipoweza kupata dk 45 kamwe usimtumie video kwani hata kabla hujatuma video au link hakikisha amefungulia njia maana yake anatakiwa kujua aende kuangalia ni nini au video husika mfano tofauti ya Bf suma na kampuni nyingine. Asipoangalia video atakusumbua.
  3. Semina ya nyumbani (home party): semina hii unaweza kuifanya nyumbani kwako au kwa mtu unayetaka kumuelimisha biashara. Kila mtu ana sebule (sitting room) lakini wengi wanatumia sebule kuongelea mambo mengine lakini siyo biashara. Lengo ni kubadilisha sebule yako au ya mtu wako iwe ni mahali mnapoweza kuongelea biashara. Unaweza ukatumia Bright Future Magazine, au flash yenye video. Ili semina hii ya nyumbani ifanikiwe sana semina hii haitakiwi kuzidi watu 10. Ni vizuri kuwa na kahawa zetu ambazo watu watakunywa unaweza ukawa na karanga pia. Sebule ni sehemu ambayo ni salama sana na watu watakuelewa sana. vifaa vya kuwa navyo:
  • Flash
  • Magazine
  • Kahawa
  • Sabuni
  • Cool roll
  • Usisahau kuwa na shuhuda kwenye simu kwani umeme waweza katika.
  • Lazima uwe na diary kwa ajili ya kupanga appointment.
  • Lazima uwe na fomu ya ushindi.

KUMBUKA

Lengo kubwa la kuelimisha mtu biashara ni kupanga mkutano mwingine (PAMBAM). Kwenye kila mkutano ambao umekutana na huyo mtu hakikisha unapanga naye huo mkutano. Unapofanya semina yeyote iwe ni ukumbini, nyumbani au one on one (mtu mmoja mmoja) lengo kuu ni kupanga naye mkutano au semina nyingine (PAMBAM) panga mkutano baada ya mkutano.

Pia lengo jingine kuu ni kuhakikisha mtu ameondoka na bidhaa yeyote moja kwa bei ya punguzo mfano: sabuni, kahawa, cool roll. Unapoanza kumuelimisha mtu biashara kwanza anza kumuelimisha kwanini wewe unafanya biashara? Kama hujui lazima ujue kwanini unafanya biashara. Watu wanajiunga sio tu kwa sababu wameielewa biashara ila kwanini wewe unafanya biashara? Pia hakikisha unaelezea ndoto zako na unazionyesha baada ya hapo muulize ndoto zake ni zipi?

Ni vizuri kujua ndoto za watu unaowaelezea biashara hii itakusaidia kuelimisha jinsi atakavyo timiza ndoto zake kupitia hii biashara. FACT TELLS, STORY SALES, Twakimu zinaongea lakini shuhuda zinauza. Tumia shuhuda za bidhaa kila unapomuelimisha mtu kuhusu bidhaa. Watu wanaelewa Zaidi shuhuda kuliko maelezo ya bidhaa, shuhuda hazisahauliki ila Takwimu zinashaulika. Takwimu hazigusi hisia lakini shuhuda zinagusa hisia. Watu huwa wanafanya maamuzi hisia zao zinapoguswa ila siyo kwa sababu wameelewa Takwimu.

Baada ya kumuelimisha mtu biashara muulize amependa nini biashara au bidhaa? MSIKILIZE. Chochote ataakacho kuwambia mpe hadithi/ushuhuda wa mtu anayeendana na yeye.

Mfano: Mwanafunzi mpe hadithi ya mwanafunzi ambaye amefanya vizuri katika biashara. Mfanyakazi mpe hadithi ya mfanyakazi ambaye amefanya vizuri katika biashara. Mwalimu mpe hadithi mpe hadithi ya mwalimu aliyefanya vizuri. Mzazi mpe hadithi ya mzazi aliyefanya vizuri. Mama wa nyumbani mpe hadithi ya mama wa nyumbani aliyefanya vizuri. Kumbuka watu wanaelewa mifano ya watu walio kama wao.

HATUA INAYOFUATA

Mjaribu kama yuko tayari kuanza biashara sasa hivi kwa kumuuliza moja ya maswali yafuatayo:

  1. Unaanza biashara leo au kesho?
  2. Unaanza na kifurushi cha 286,000 au 186,000?
  3. Chukulia mfano wa kipimo cha 1-10 (moja maana yake umesikiliza biashara umeelewa lakini unaona huwezi kufanya. 10 maana yake umesikiliza biashara na umeielewa na uko tayari kuanza sasa hivi Wewe uko wapi?

HATUA INAYOFUATA

Baada ya hapo muulize msululu wa maswali yafuatayo:

  1. Kutokana na ulichokisikiliza au kukiangalia kama ukianza kufanya biashara hii kwa muda wa ziada wewe unataka kuingiza shilingi ngapi kwa mwezi ili biashara hii iwe ya maana sana kwenye maisha yako? MSIKILIZE. Akijibu andika chini kiasi anachotaka kuingiza (Swali litakusaidia kujua mtu wako anataka kuingiza shilingi ngapi katika biashara pia litakujuza namna anavyoichukulia biashara ki ukubwa au ki udogo.
  2. Ili uweze kuingiza (sema kiasi cha fedha alichokwambia kwenye swali la kwanza) upo tayari kuwekeza kwenye masaa mangapi kwa siku pamoja na weekend zake? MSIKILIZE. Akijibu muulize swali lifuatalo.
  3. Ili uweze kuingiza (sema kiasi cha fedha alichokwambia kwenye swali la kwanza) kwa kuwekeza masaa jibu alilokupa kwenye swali la pili kwa siku pamoja na weekend upo tayari kufanya hivyo kwa muda gani au miezi mingapi? Swali la pili litakusaidia kujua muda wa kujitoa (commitment) kwake kufanya kazi ili kukamilisha ndoto yake ya kipato. Swali la tatu linakusaidia kujua uwezo wake wa kuwa na mwendelezo au uvumilivu wake hadi kukamilisha ndoto yake.
  4. Ili uweze kuingiza (sema kiasi cha fedha alichokwambia kwenye swali la kwanza) kwa kuwekeza masaa jibu alilokupa kwenye swali la pili kwa siku pamoja na weekend kwa kujitoa kwa miezi? Jibu swali la tatu. Upo tayari kuwafikia watu 150-200.
  5. Ili uweze kuingiza (sema kiasi cha fedha alichokwambia kwenye swali la kwanza) kwa kuwekeza masaa jibu alilokupa kwenye swali la pili kwa siku pamoja na weekend kwa kujitoa kwa miezi kama alivyojibu swali la nne? Kama upotayari kuwafikia watu 150-200. Upo tayari kufundishika?
  6. Kama nikikufundisha kuingiza (kiasi ulichosema kwenye swali la kwanza?) kwa kuwekeza masaa (kama alivyosema kwenye swali la pili), kwa kujitoa kwa miezi (kama alivyosema swali la tatu), kwa kujitoa kwa miezi (kama alivyojibu swali la nne), na kama unafundishika? Uko tayari kuanza biashara sasa hivi? MSIKILIZE. Akisema ndio muulize unaanza na kifurushi cha 286,000 au 186,000? Akisema hapana muulize kitu gani unahitaji kufahamu Zaidi ili uweze kuanza sasa hivi? Msikilize, Akijibu hapana. Muulize tena, kwa hiyo kitu gani unataka kukielewa ili uanze biashara leo?

Kumbuka mtu ili aweze kufanikiwa sana katika hii biashara anatakiwa ajitoe masaa 2 kwa siku na kujitoa kwa miezi angalau 18 na kuendelea.

Mwandae mtu wako uliyemwelimisha biashara namna ya kukabiliana na waiba ndoto. Baada ya kumuelimisha mtu biashara tegemea atakaporudi nyumbani ataenda kuomba ushauri au kuwahadithia watu wengine ambao hawajapata taarifa za kutosha juu ya biashara ya BF Suma. Kumbuka wewe umeona, umeuliza maswali, umenusa, umegusa. Maamuzi yako juu ya biashara yametokana na kuona picha kubwa. Mtu anapotoka kwenda kuwahadithia watu atawaonyesha picha ndogo na wengi wao hawatamuelewa na hivyo watamkatisha tamaa maana hasi ina nguvu kuliko chanya. Mwaandae mtu uliyemuelimisha biashara kisaikolojia kwa kumwambia maneno yafuatayo:

“Najua umeipenda biashara na umeifurahia najua utatoka hapa na kwenda kuwahadithia wengine ulichojifunza tegemea kukataliwa na kukatishwa tamaa. Taarifa nilizokupatia ni kamilifu, zinajitosheleza, taarifa utakazoenda kuwaambia hazijitoshelezi na haziko kamili kwa hali hiyo watu watakukatisha tamaa kwa sababu hawatakuelewa na watu hao ni watu wa karibu kama vile baba, mama, kaka, dada, mjomba, rafiki, mpenzi. Kama unataka kumuelimisha mtu biashara niunganishe naye nimuelimishe biashara kwa sababu mimi nina taarifa zote, pia unaweza kutumia vifaa vifuatavyo kumuelimisha, mtumie link ya biashara inayolipa, au magazine, au flash au mpatie kipeperushi kitakachomsaidia kuelimishia watu au mpatie sample ya bidhaa coll roll, sabuni, kahawa nk.

Kwa kufanya hivyo utakuwa umemlinda mtu wako asiharibiwe na kuibiwa na waiba ndoto waliyoko huko mtaani. Hakikisha unamuhami mtu wako na vifaa vitakavyo mlinda mtu wako.

HATUA INAYOFUATA

PAMBAMU

Panga mkutano baada ya mkutano. Hakikisha unapanga mkutano mwingine na mtu uliyemaliza kumuelimisha biashara. Kila unapokutana na mtu moja panga naye mkutano mwingine.

MBINU YA KUJIBU MASWALI YA FEEL, FELT, FOUND (NINAKUELEWA, NA MIMI NILIKUWA KAMA WEWE, LAKINI NIKAGUNDUA)

Mtu anapoonyesha wasiwasi/hofu kwa mfano: nitapataje wateja? Nitauzaje? Nitaumuuzia nani? Njia gani nitatumia kuuza? Mimi sijui kuongea kama wewe? Sina uzoefu na biashara hii. Mjibu hivi sawa, NIMEKUELEWA, NA MIMI NILIKUWA KAMA WEWE, LAKINI BAADA KUJIUNGA NIKAGUNDUA kwamba kuna madarasa ya kufundishwa namna ya kupata wateja, kuuza, njia za kutumia wateja. Kwa hiyo kitu cha kwanza nikuanza baada ya kuanza utajifunza na wewe utaweza.

Katika biashara hii hakuna kitu ambacho utakifanya ambacho aliyekutangulia hajakifanya hivyo kabla hujafanya muulize aliyekutangulia katika biashara (upliner). Kitu chochote hasi mwambie mtu wa juu au mtu aliyekutangulia katika biashara kwa yeye atakusaidia kutatua. Kamwe usimwambie mtu aliyechini (downline) maana utamkatisha tamaa nayeye hana majibu.

Ni kawaida kukata tamaa katika biashara. Nitajua umekata tamaa pale ambapo utakuwa hupokei simu zangu, huji kwenye mikutano na utakuwa na visingizio vingi.  Ukiwa katika hali ya kukata tamaa wewe ni mtu wa aina gani kati ya hawa:

  1. Mtu ambaye unapenda kukumbushwa kwanini ulianza biashara hii kwa hiyo niendelee kukusumbua mara kwa mara.
  2. Mtu ambaye huwa hupendi kusumbuliwa unapokuwa umekata tamaa kwa hiyo nikuache hadi pale wewe mwenyewe utakapoamua kurudi

Wewe ni mtu wa aina gani kati ya hawa namba moja au mbili?

Hakikisha kila mwanzo wa mwezi umepewa plan na kiongozi wako (upliner) hii itakusaidia kujua unataka kufanya nini? Na hii itakusaidia kupanda rank za bf suma kwa haraka.

Ni uwezo wako wa kuwasaidia watu wengine kufanya biashara kirahisi kama wewe. Mfumo wa biashara ya BF Suma unampa mtu fursa mbili kubwa ambazo fursa ya kwanza ni kuuza bidhaa na kutatua changamoto za watu za Kiafya. Fursa ya pili ni kutatua changamoto za watu za kiuchumi.

Kifupi BF Suma inakupa nafasi ya kuuza bidhaa na kuuza biashara. Unapomuunganisha mtu kwenye biashara maana yake umemuuzia biashara yaani amenunua kwako biashara na BF Suma inakulipa kwa kumuuzia mtu mwingine biashara kwa hiyo hakikisha mtu anapojiunga anaweza kujitegemea haraka kwa kufanya mambo marahisi marahisi ambayo yatampa matokeo/mafanikio makubwa.

Watu uliowaunganisha katika biashara watafuata unachokifanya siyo unachokisema. Na kama unachokifanya ni kigumu sana basi hawezi kufanya. Na wasipoweza kufanya usichoweza kufanya maana yake ni kwamba wewe hauna biashara. “Mafanikio katika BF Suma yanakuja kwa kuwafanya watu wengi kufanya vitu vidodgo vidogo kila siku”

Mambo madogo madogo ya kufanya kila siku ni kama kuongeza orodha yako watu wawili kila siku, kupiga simu kwa kufuata utaratibu maalumu (script), kuelimisha kwa kutumia magazine, kuwahadithia hadithi, kuwaelimisha watu kwa kutumia video au flash, kufuatilia watu uliowaelimisha au wauzia bidhaa, kuangalia picha za ndoto zako, kusoma malengo yako kila siku, kusoma kadi yako ya malengo (index card), kufanya affirmation.

Unapotumia vifaa utaweza kuwasaidia watu wengi kufanikiwa katika biashara. Kwa sababu kutumia vifaa ni njia rahisi sana na kila mtu anaweza kufanya, na kila mtu anaweza kufanya katika biashara hiyo ndio inaitwa dublication maana yake fuata utaratibu uliowekwa katika kitabu hiki.

Mtu akikwambia sina muda, muulize: huna muda wa kufanya nini? Huna muda wa kutengeza pesa au huna muda wa kutumia pesa?

MUDA FEDHA KAZI
Hapana Hapana Wanafunzi, wafanyakazi
Ninao Hapana Wasio na kazi
Hapana Ninao Watu wenye biashara ndogo
Ninao Ninao Wafanya biashara wakubwa, wawekezaji na networkers

Wewe ni yupi kati ya hao?

SABABU 8 KWANINI WATU WANAFELI KWENYE BIASHARA YA MTANDAO

  1. Hawaipi uzito biashara
  2. Mashaka
  3. Hawawekezi muda wao kufundishwa namna ya kuielewa biashara vizuri
  4. Wanahisi ni biashara ya kunufaika haraka
  5. Hawana dira
  6. Hawajui namna ya kuwasilisha biashara
  7. Hawaangalii mbali
  8. Watu wanaofeli hawana maono.

KANUNI YA KUTAJIRIKA:  JIFUNZE, FUNDISHA FANYA

  1. Matajiri Wanajifunza Kuuza, Wanafundisha Kuuza, Wana-Uza.
  2. Matajiri Wanajifunza Kuongoza, Wanafundisha Kuongoza, Wana-Ongoza.
  3. Matajiri Wanajifunza Kujenga Team, Wanafundisha Kujenga Team, Wanajenga-Team.
  4. Matajiri Wanajifunza Kupambana Na Changamoto, Wanafundisha Kupambana na Changamoto Wanapambana na Changamoto.

NAMNA YA KUMSAIDIA MTU AWEZE    KUANZA BIASHARA SAHIHI AU ATUMIE BIDHAA HADI MWISHO.

PART 1: MUONYESHE KWANZA MAAMUZI ALIYOYAFANYA NI SAHIHI

  • Mtu anapoanza biashara MPONGEZE kwa maamuzi yake aliyoyafanya na muonyeshe kwamba MAAMUZI hayo yatamsaidia KUKAMILISHA ndoto zake na maono yake. Mfano: Hongera sana kwa kuanza biashara na kifurushi cha (TAJA KIFURUSHI ALICHOANZA NACHO). Hakika huu uamuzi wa leo unaenda KUBADILISHA MAISHA YAKO na utasaidia KUKAMILISHA NDOTO ZAKO. Kuna watu wengi wamebadilisha maisha yao kupitia biashara hii mhadithie hadithi yako, hadithi ya Upliner wako aliyefanikiwa, msikilizishe video ya huyo kiongozi alivyokuwa.

PART 2: MTENGENEZEE MATARAJIO SAHIHI KATIKA BIASHARA

  • Kufanikiwa au kushindwa katika hii biashara kuna kutegemea wewe mwenyewe 100%. Wewe ndiye UTAKAYE SABABISHA UFANIKIWE AU USHINDE katika hii biashara.
  • Kazi yangu ya kwanza kubwa kwako ni KUKUONGOZA SIYO KUKUFANYIA, NIPO HAPA TUFANYE KAZI PAMOJA SIYO KUKUFANYIA KAZI.
  • Kazi yangu ya pili ni KUKUFANYA UJITEGEMEE MAPEMA SANA.
  • Kila kitu katika hii biashara UTAJIFUNZA NA UTAJUA. Nachotaka kwako UWE TAYARI KUJIFUNZA NA UWE MWANAFUNZI.

PART 3: KWENYE BIASHARA KUNA KUANGUKA NA KUSIMAMA

  • Utakapokuwa unaendelea kujenga biashara yako kuna KUANGUKA NA KUSIMAMA, KUNA FURAHA NA KUKATA TAMAA.
  • Nitajua kwamba unakata tamaa ikiwa utakuwa HUPOKEI SIMU NIKIKUPIGIA, UTAKUWA HUJI KWENYE MIKUTANO, UTAKUWA NA MASHAKA, UTAKUWA NA VISINGIZIO. Ikitokea hiyo hali kwako na wewe siyo wa kwanza kupata hali hiyo. UNATAKA NIENDELEE KUKUTAFUTA NA KUKUSUMBUA AU NIKUACHE??

PART 4: M-CONNECT MTU WAKO NA VYANZO VYOTE VYA TAARIFA

  1. Video za kuelimisha watu biashara
  2. Karatasi ya bei za bidhaa
  3. Anajua website ya kampuni (bfsuma.com)
  4. Anajua Website ya timu (www.dreamteamtz.com)
  5. Anajua page na Instragram ya BF SUMA na amei-follow (bf suma)
  6. Hakikisha mtu wako ana-follow page za timu (Dream Team) facebook, instragram na YouTube
  7. Muunganishe na group la Telegram (Dream Team)
  8. Mpe ratiba za mikutano na mafunzo
  9. Muunganishe kwenye Touch bf suma, report bf suma.

KUMBUKA

Lengo lako ni kumfanya ajitegemee haraka.  Msaidie aweze kujiunga na Touch bfsuma

PART 5: HAKIKISHA MTU WAKO ANAVIFAA VYA BIASHARA

  1. Magazine
  2. Daftari za orodha
  3. Diary
  4. Vision book
  5. Daftari la notes
  6. Index card
  7. Ushauri wa Afya
  8. Hatua za Ushindi business Guide
  9. Karatasi ya bei za bidhaa
  10. Video za shuhuda za bidhaa (www.brightfutureteam.com)
  11. Anazo shuhuda za waliofanya vizuri katika biashara

PART 6: HAKIKISHA MTU WAKO ANAJUA NAMNA SAHIHI YA KUALIKA

Hii itamsaidia kutokupoteza watu wake wazuri wa awali

PART 7: SKILLS ZA KUFANYIA KAZI

  1. Kuandika orodha ya watu kuanzia 150: Muonyeshe video ya kuandika iliyoandaliwa na mimi Yusuph Mbarouk.
  2. Ajue bidhaa zote za BF Suma: Muonyeshe video ya bidhaa zilizoandaliwa na mimi Yusuph Mbarouk
  3. Edification: Muonyeshe video ya namna ya kufanya edification iliyoandaliwa na mimi Yusuph Mbarouk
  4. Namna sahihi ya kualika: Muonyeshe video ya namna ya iliyoandaliwa na mimi Yusuph Mbarouk
  5. Ajue aina 4 za watu wa kuepuka

BONUS VIDEO ZA KUJIFUNZA

  1. Hatua 5 za mafanikio
  2. Maadui 4 katika biashara
  3. Kwanini utumie vifaa katika kuelimisha watu?
  4. Umuhimu wa shuhuda katika biashara yako?
  5. Kwa nini BF SUMA ni kampuni bora?
  6. Mfumo wa malipo
  7. Aina 4 za watu wa kuepuka
  8. How to build your network business?
  9. Leader talk with John Mutua (Manda-Senior crown leader)
  10. Goal setting by Mutua Manda (Senior crown leader)
  11. Motivation on how to succeed in BF SUMA by John Mutua Manda (Senior crown leader)

PART 8: KUZINDUA BIASHARA

  • Muulize mtu wako WEWE NI MTU WA AINA GANI? UNATAKA KWENDA SPEED OR SLOW?
  • Mtu wa speed yuko tayari KUFANYA CHOCHOTE:-
  1. Anafundishika haraka na akipewa kazi anaifanya haraka
  2. Yuko tayari kuwekeza kwenye social media. Muda wake wa kufanya biashara ni masaa 2 na kuendelea
  • ANZA KUFANYA NAYE KAZI
  1. Apate mteja wake wa kwanza (Anzeni kwa pamoja kuongea na wagonjwa wake, akufanyie edification)
  2. Apate miguu yake 3 ya kwanza (AWATUMIE VIDEO WATU SAHIHI, akufanyie edification ili uwa-close)
  • Apate bonus yake ya kwanza
  1. Apate marafiki kwenye timu
  2. Apate Recognition ya kwanza kama vile special case bonus, Queen of sales, King of sales, Rank mpya nk
  3. Ahudhurie semina yake kubwa ya kwanza
  • APIGIE SIMU WATU WAKE ANAOFAHAMIANA NAO, AWAELIMISHE WATU JUU YA BF SUMA, AWATUMIE VIDEO ILI WAJUE ANACHOKIFANYA. HAO WANAWEZA KUWA WATEJA AU KUJIUNGA NA BIASHARA AU WAMUUNGANISHE NA WATEJA.

18 thoughts on “Hatua Za Mafanikio”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *