NAMNA YA KUWAALIKA WATU ILI WAJE KUJIFUNZA BIASHARA AU KUWAELIMISHA JUU YA BIDHAA.
NAMBA 1
JINSI YA KUWAPIGIA SIMU KUWAALIKA WATU KUJA KWENYE SEMINA AU KUWAELIMISHA
- Kuwaalika mteja wako ni moja ya stadi muhimu sana ili waweze kufanikiwa sana kwenye biashara yako
- HAKIKISHA UNA ORODHA YA WATU 250 unaotaka kuwafikishia ujumbe wa BF SUMA
- Usiwe na papara, fuata utaratibu wa kupiga simu na watu wako watakuelewa tu
- Ni kawaida kwa mtu unapoanza kukosea hapa na pale ila ukirudia mara kadhaa utakuwa vizuri, kila mmoja alianza akiwa hajui ila kwa kurudia rudia akawa anajua, UTAWEZA
- Lengo la kuwalika/KUPIGA SIMU NI KUMPA MTU HAMASA (CURIOSITY)
- MTU WAKO ANAPOKUJA /UNAPOONANA NAE TUMIA VIFAA/VYENZO/TOOLS KUMUELIMISHA KUHUSU BF SUMA, USIMWELEZE KWENYE SIMU HATAELEWA KABISA. VIFAA/VYENZO/TOOLS NI KAMA MAGAZINE, VIDEO ZA FURSA. Tembelea Website ya Kiswahili ya www.dreamteamtz.com, VIDEO ZA USHUHUDA, MAGAZINE SOFT COPY
- MTU ANAPOKUWA NJE YA MKOA TUMIA VIDEO/MTUMIE MAGAZINE KWA WHATSAPP
Lengo si kumweleza na kumuelimisha kuhusu BF SUMA kwenye simu, ukifanya hivyo mambo yafuatayo yatakutokea: Utatumia nguvu kubwa sana na vocha nyingi kumueleza hadi aelewe na kama akikuelewa atakuambia yeye hawezi kuwaeleza watu wengine kama wewe hadi ajifunze kwanza
MASWALI AMBAYO UTAULIZWA NA WATU UNAPOWAPIGIA SIMU NA NAMNA SAHIHI YA KUJIBU
SWALI 1: Ni biashara gani? Au si uniambie tu kwenye simu?
JIBU: KUNA VITU VYA KUONA NA KUJIELIMISHA, NIKIKUELEKEZA KWENYE SIMU HATA HUWEZI KUNIELEWA, VILEVILE BIASHARA HII INAWEZA IKAKUFAA AU ISIKUFAE, NINAPENDA TUONANE, NIKUONYESHE PICHA KUBWA ILI UFANYE MAAMUZI SAHIHI. MUDA WAKO UKOJE ILI TUWEZE KUONANA.
SWALI 2: Hii ni biashara kama ya Forever au Aim Global Au Ole frem?
SIYO KILA MTU ANAYEKUULIZA SWALI HILI ANA MTAZAMO HASI JUU BIASHARA YA MTANDAO. HAKIKISHA UNAJUA KWANINI ANAKUULIZA SWALI HILO ACHA KUJITETEA NA KUHISI AMEKUULIZA HIVYO KWA SABABU YUKO HASI.
JIBU: NDIO, MUULIZE UMEWAHI KUFANYA BIASHARA YA AINA HII AU UNAMFAHAMU MTU ALIYEWAHI KUFANYA BIASHARA KAMA HII? MSIKILIZE ILI UJUE KWANINI AMEKUULIZA SWALI HILI? AKUAMBIE CHANGAMOTO ALIZOPATA HALAFU JIBU: UKIONA BIASHARA ISIYO NA CHANGAMOTO HIZO BADO UPO TAYARI KUJIELIMISHA? MSIKILIZE…MUULIZE, SIKU IPI NI NZURI TUONANE ILI NIKUELIMISHE?
NAMBA 2
UFUATAO NI UTARATIBU RAHISI WA KUMUALIKA MTU
- JIAMINI: Unayeongea nae hajui kama unakosea au unapatia
- MTAJE KWA JINA: Helloo Shukran
- MUULIZE KAMA YUPO SEHEMU NZURI UONGEE NAYE: Una dakika moja ya haraka tuongee?
- MSIFIE: Nimekupigia simu hii kwa sababu wewe ni muelewa sana
- ONYESHA THAMANI KWA KUMUULIZA: KWA MFANO. UKIONA BIASHARA INAYOWEZA KUKUONGEZEA KIPATO CHA ZIADA BILA KUATHIRI SHUGHURI ZAKO NA KWA MTAJI MDOGO, UNAWEZA KUJIELIMISHA UONE KAMA ITAKUFAA?
- ONYESHA KAMA HUMUHITAJI: KUNA BIASHARA NIMEIANZA AMBAYO INAWEZA KUINIONGEZEA 100,000 HADI 500,000 KWA WIKI NA KWA MTAJI MDOGO SANA, INAWEZA IKAKUFAA AU ISIKUFAE. IKIKUFAA NI VYEMA NA ISIPOKUFAA NI VYEMA PIA.
- CHAGUA NJIA SAHIHI YA KUMUELIMISHA, UNAYOPENDA: KWA SABABU KUNA VITU VYA KUONA, KUJIELIMISHA NA KUONJA. MFANO NIKUKUALIKA KWENYE SEMINA KESHO SAA 8 MCHANA HAPA KIMARA STOPOVER, SHANGO HOUSE GOROFA 1, UNAWEZA KUJA NIKUELIMISHE UONE KAMA NI KITU KINACHOKUFAA?
KAMA YUKO NJE YA MKOA
KABLA HUJATUMA VIDEO HAKIKISHA MTU ANA DK 45 HADI LISAA 1 LA UTULIVU. UNAPOPIGA SIMU LENGO LAKO NI KUPATA MIADI YA YEYE KUANGALI VIDEO SIYO KUMTUMIA VIDEO.
Kwa mfano nikukutumia Link ya video fupi kwa whatsapp inayoelezea kila kitu unaweza kuiangalia uone kama itakufaa? (unaweza kumtumia link akaangalia moja kwa moja Youtube au unaweza kumwambia apakue telegram ili umtumie kupitia telegram aangalie video nzima)
KAMA UNATAKA KUONANA NAE UNASEMA:
Muda wako ukoje twaweza kuonana nikuelezee kila kitu, kawaida ninaonana na watu ofisini kwangu KIMARA STOPOVER, SHANGO HOUSE GOROFA 1 kila siku saa 8 mchana hadi saa 11 jioni. Je, huu ni muda mzuri kwako?
NAMBA 3
JINSI YA KUWALIKA RAFIKI ZAKO NA NDUGU UNAOELEWANA NAO SANA/ ULIONAO KARIBU
(NJIA YA KIBABE)
Helloo Shukran una dakika moja ya haraka tuongee?
Siku ya alhamisi una kitu gani ambacho unakifanya kinachoweza kukuingizia 500,000 kwa wiki?
Hakuna
Ninakuwalika siku hiyo kwenye semina itakayoweza kukuingizia 500,000 KWA WIKI KWA KUTUMIA MUDA WAKO ZIADA NA KWA MTAJI MDOGO. KUTAKUWA NA WAJASIRIAMALI WALIOFANIKIWA
NI BIASHARA GANI HIYO?
Kuna vitu vya kuona na kujielimisha, nikikuambia kwenye simu hata huwezi kunielewa. Ukija kwenye semina utapata picha kubwa.
Kwa hiyo utakuwepo alhamisi saa 8 ili nikuwekee nafasi?
NAMBA 4
JINSI YA KUWALIKA WATU WALIOKUZIDI KIUCHUMI, WENYE USHAWISHI MKUBWA AU WALIOFANIKIWA SANA
MFANO: WACHUNGAJI, WABUNGE, MA CEO, MATAJIRI NK
Lengo la kumpigia simu mtu huyu ni ili upate wasaa wa kukutana naye umuelimishe bidhaa zetu na mfumo wa malipo ili ajiunge au anunue bidhaa au akukutanishe na watu ambao wanaumwa ili wawe wateja wako au akukutanishe na watu watakaojiunga kwenye biashara yako
KUMBUKA: MTU HUYU UNAWEZA KUONANA NAYE HUKO ALIKO
NAMNA YA KUMPIGIA SIMU
HELLOO (MSALIMIE KUTOKANA NA NAFASI ALIYONAYO)
HELLOO!! BABA MCHUNGAJI SHIKAMOO. UNA DAKIKA MOJA YA HARAKA TUONGEE KUNA KITU CHA MUHIMU SANA NINATAKA UNISAIDIE. KUNA BIASHARA NIMEIANZA. KWA SABABU WEWE UNAKUTANA NA WATU WENGI NA UMEONA VITU VINGI KULIKO MIMI. NILIKUWA NINAOMBA UNISAIDIE KUNISHAURI NA KUNIKUTANISHA NA WATU AMBAO NITAWAHUDUMIA NA KUWASAIDIA KUPITIA BIASHARA HII. SASA KWA SABABU KUNA VITU VYA KUONA, KUJIELIMISHA NA KUONJA NIKIKUELEZEA KWENYE SIMU HATA HUWEZI KUELEWA. NINAOMBA NIPATE WASAA NA WEWE WALAU DK 30 ENEO AMBALO LITAKUWA CONFOTABLE KWAKO ILI NIWEZE KUKUONYESHA, KUKUONJESHA NA KUKUELIMISHA, SIKU GANI ITAKUWA NI NZURI KWAKO ILI TUONANE.
AKICHAGUA MUDA MWAMBIE NITAKUJA NA BUSINESS PARTNER WANGU ILI UTUSHAURI KWA PAMOJA.
NAMBA 5
NAMNA YA KUPATA WATU ZAIDI
KILA UNAEMUELIMISHA BF SUMA ANA NAFASI YA KUKUPA WATEJA (WAGONJWA ANAOWAFAHAMU) NA WATU WATAKAO JIUNGA KAMA UKIJUA NAMNA YA KUMUOMBA
JINSI YA KUPATA WATEJA ANA WATU WENGI ZAIDI KUTOKA KWA KILA MTU UNAE MFANYIA SEMINA NA JINSI YA KUWAPIGIA SIMU WATU HAO ULIOPEWA NA KUWAALIKA KWENYE SEMINA AU KUWAELIMISHA
- Je, unajua kila mtu unayemfanyia semina BF SUMA ana watu nyuma yake? Mtu mmoja anaweza kukutanisha na watu wengine wengi ambao watakuwa wateja wako wakubwa wa bidhaa au watakaojiunga kwenye biashara.
- Skills hii ya kuwatumia unaowafanyia semina au wateja wako kukuunganisha na watu wengine itakusaidia kupata watu wengine wapya kila siku wa kuwauzia bidhaa na kuwafundisha biashara.
- Unapomfanyia semina mtu mmoja nyuma yake ona kuna watu zaidi ya 250
- KAMWE USIWE KAMA WATU WENGINE ambao wanapofanya semina kwa watu wanamuacha anaondoka hivi hivi bila ya kuchukuwa watu wake ambao anapenda kujiongezea kipato cha ziada au wenye matatizo ya kiafya ambao bidhaa zitawasaidia.
- KUMBUKA: Mtu unayemfanyia semina ni daraja la kukutanisha na watu wengine wenye matatizo ya kiafya na wanaopenda kujiongezea kipato hivyo leo nakufundisha jinsi mtu huyo atakavyokupa watu wengine watakao kuwa wateja wako na watakaojiunga na wewe
BAADA YA KUFANYA SEMINA KWA MTU/WATU
Hakikisha amekupa namba na amekutambulisha kwa watu wake anaodhani wanapenda pia kujifunza zaidi juu ya biashara inayoweza kuwaongezea kipato cha ziada na bila kuwathiri shughuli zao
Pia hakikisha amekupa tena namaba za watu ambao anadhani wakipata ELIMU juu ya bidhaa za BF SUMA watatua changamoto zao za KiafyaANAKUPAJE NAMBA ZA WATU ANAOWAJUA WENYE CHANGAMOTO ZA KIAFYA NA WANAOTAKA KUJIONGEZEA KIPATO?
NI RAHISI SANA: Mtumie jumbe zote mbili kwenye simu yake UJUMBE WA AFYA NA UJUMBE WA BIASHARA (JUMBE ZINAJIELEZA ZENYEWE) Mwambie AWATUMIE WATU WAKE HALAFU AKUPE MAJINA NA NAMBA ZAO, kwa yeye kuwatumia ujumbe anakuwa amekutambulisha katika bidhaa zako utakazoanzia na utaongeza fedha kidogo iliyobaki kukamilisha fedha ya kuwanzia na hongera umepata mteja wa kuwanza nae
JINSI YA KUJIBU CHANGAMOTO KATIKA ZOEZI LA KUCHUKUWA NAMBA ZA WATEJA NA NAMBA ZA WATU WAKE WATAKAOFANYA BIASHARA
- HADI NIONGEE NAO KWANZA NDIO NIKUPATIE NAMBA
JIBU: Mimi nina uzoefu na ninazijua bidhaa vyema na ninajua kuelezea vizuri zaidi yako, wewe ukiulizwa maswali mawili tu hutoweza kujibu na mtu atakuona hujui hivyo hatofanya maamuzi mazuri, hivyo mimi ninajua zaidi nitakusaidia kuongea nao na ujumbe niliokutumia ukiwatumia wataelewa huna haja ya wewe kuongea sana.
- NIKIENDA NYUMBANI NITAKUTUMIA MAJINA USIWE NA HOFU HII SIMU YANGU HAINA WATU HADI NICHUKUE SIMU KUBWA HALAFU NATAKA NICHAGUE WATU
JIBU: Nakuelewa sana ila nimeongea na watu wengi sana wanapotoka hapa mambo yanakuwa mengi sana, na mimi ninakuwa na watu wengi sana, najua utakuwa nao wachache hapo ulipo unaowakumbuka tuanze na hao. Lengo ni kuwaelimisha kama nilivyokuelimisha, nao wataamua wenyewe.
- SASA IKITOKEA WATU WANGU WAKANUNUA KABLA MIMI SIJAJIUNGA AU WAKAANZA KABLA MIMI SIJAANZA
JIBU: Mtu anapoanza maana ataanza na timu sasa na unapoanza na timu maana yake mwisho wa mwezi utapata fedha/hivyo hivyo itakusukuma kupata fedha haraka ya kuanza kwa sababu unajua lazima mwisho wa mwezi utapata fedha, na kama mtu wako akinunua maana yake umepunguza gharama ya kujiunga maana yake mtu wako aliyenunua bidhaa zake tutazijumlisha kwako.
UJUMBE WA BIASHARA KWA AJILI YA WATU WAKE WANAOPENDA KUJIONGEZEA KIPATO (FURSA)
Habari natumaini ni kwema? Kuna Rafiki yangu anaitwa (weka jina lako na namba yako MFANO: YUSUPH – +255 718 172 170) Amenielimisha biashara ambayo inaweza kuniingizia kipato cha ziada cha 100,000 hadi 500,000 kwa wiki bila kuathiri shughuli zangu kwa mtaji mdogo sana nimemwomba akupigie naomba umsikilize, akuwalike kwenye semina ukae nae uone kama itakujaa. AHSANTE (WEKA JINA LAKE LINALOJULIKANA NA NAMBA YAKE) MFANO SHUKRAN 0676 114316)
UJUMBE KWA WATU WENYE CHANGAMOTO ZA KIAFYA AMBAO BIDHAA ZA BF SUMA ZITAWASAIDIA, HAWA WATAKUWA NI WATEJA WAKE WA KWANZA AMBAO UMEMSAIDIA KUONGEA NAO
Habari natumaini ni kwema? Kuna rafiki yangu anaitwa (WEKA JINA LAKO NA NAMBA YAKO YA SIMU, MFANO: YUSUPH +255 718 172 170) Amenishirikisha dawa nzuri za Kiafya kutoka MAREKANI ambazo zimewasaidia watu wengi sana wenye changamoto za Kiafya, nimemuomba akupigie simu akuelimishe, naomba umsikilize naamini hizo dawa zitakusaidia sana. AHSANTE (WEKA JINA LAKE LINALOJULIKANA NA NAMBA YAKE)
NAMBA 6
JINSI YA KUWAPIGIA SIMU WATU HAO ULIOPEWA NA KUWAALIKA KWENYE SEMINA AU KUWAELIMISHA
HAKIKISHA AMETUMIWA UJUMBE WA KUKUTAMBULISHA
HATUA
- JIAMINI
- MTAJE KWA JINA: Hello Shukran
- JITAMBULISHE: Unaongea na Mbarouk namba yako amenipa Shukran bila shaka unamfahamu na bila shaka alikutumia ujumbe kuwa Mbarouk atakupigia.
- MSIFIE: Shukran aliniambia wewe ni mtu wake wa karibu na mwelewa sana
- ONYESHA THAMANI: vilevile aliniambia kwamba kama ukiona biashara inayoweza kukuongeza kipato cha ziada bila kuwathiri shughuli zako na kwa mtaji mdogo unaweza kujielimisha uone kama itakufaa
- ONYESHA KAMA HUMUHITAJI: Nilimuelimisha Shukran biashara inayoweza kuniingizia 100,000 hadi 500,000 kila wiki kwa mtaji mdogo akawa ameipenda sana na akaomba nikupigie nawe pia nikuelimishe huenda itakufaa au isikufae ila kwa sababu kuna vitu vya kuona na kujielimisha, mfano nikikuwalika ofisini kwangu hapa KIMARA STOP OVER, SHANGO HOUSE GOROFA YA 1 leo saa 8 mchana unaweza kuja kujielimisha uone kama itakufaa au laa?
KAMA YUKO MBALI NA HAWEZI KUJA TUMIA WHATSAPP VIDEO, SEMA
Nilimuelimisha Shukran biashara inayoweza kuningizia 100,000 hadi 1,000,000 kila wiki kwa mtaji mdogo akawa ameipenda sana na akaomba nikupigie nawe pia nikuelimishe huenda itakufaa au isikufae, ila kwa sababu kuna vitu vya kujielimisha mfano nikikutumia video fupi ya whatsapp unaweza kuangalia uone kama itakufaa au laa?
AU KAMA UNATAKA AJE KWENYE SEMINA, SEMA…
Nilimuelimisha Shukran biashara inayoweza kuningizia 100,000 hadi 1,000,000 kila wiki kwa mtaji mdogo akawa ameipenda sana na akaomba nikupigie nawe pia nikuelimishe mfano nikikuwalika kwenye semina leo saa 8 mchana unaweza kuja kujielimisha uone kama itakufaa?
NAMBA 7
NAMNA YA KUKUZA ORODHA YAKO NA KUPATA WATU WA KUWAAMBIA BIASHARA YAKO KILA UNAPOKUWA
Kila mahali kuna watu, popote ulipo unaweza kupata mtu atakayekuwa kiongozi mkubwa BF SUMA, usimdharau mtu usiyemjua, kila unayekutana naye ni dhahabu, unaweza kukutana na mtu mahali popote au hata kwenye mitandao ya kijamii kama vile facebook, instragram nk
Unapoonana na mtu barabarani, kanisani, msikitini, shuleni, dukani, chuoni, kwenye daladala au kwenye kituo cha mabasi tabasamu, anzisha mazungumzo yeyote muulize vitu vya kawaida, anafanya kazi gani? mwenyeji wa mkoa gani? Ana muda mrefu anaishi Dar es salaam? usione aibu kujieleza kidogo pia muulize maswali haya hapa chini ili kumpeleka kwenye biashara.
MASWALI YA MOJA KWA MOJA
- Nje na kazi yako una biashara yeyote unayofanya inayoweza kukuingizia kipato kwa muda wako wa ziada? MSIKILIZE JIBU LAKE AKIMALIZA ENDELEA KWA KUSEMA
Nimepatner na kampuni ya Kimarekani inayoitwa Bright Future sasa tunaongeza wigo wa soko hapa Dar es salaam hivyo tunatafuta watu waelewa ambao wapo chanya na wanaotafuta kujiongezea kipato kwa kutumia muda wao wa ziada kwa sababu kuna vitu vya kuona na kujielimisha namba yako ipi nzuri ili niweze kukualika kwenye semina zetu na kukutumia taarifa zaidi uone nini tunafanya na namna unavyoweza kutumia muda wako wa ziada kwa mtaji kidogo kuanzisha biashara kubwa na sisi?
- Ulisha wahi kufikiria kujiongezea kipato kwa kufanya biashara katika muda wako wa ziada? MSIKILIZE JIBU LAKE AKIMALIZA ENDELEA KWA KUSEMA
Nimepatner na kampuni ya Kimarekani inayoitwa Bright Future sasatunaongeza wigo wa soko hapa Dar es salaam hivyo tunatafuta watu waelewa ambao wapo chanya na wanaotafuta kujiongezea kipato kwa kutumia muda wao wa ziada kwa sababu kuna vitu vya kuona na kujielimisha namba yako ipi nzuri ili niweze kukualika kwenye semina zetu na kukutumia taarifa zaidi uone nini tunafanya na namna unavyoweza kutumia muda wako wa ziada kwa mtaji kidogo kuanzisha biashara kubwa na sisi?
- Kwa mfano ukiona biashara ambayo inaweza kukuongezea kipato bila kuathiri shughuli zako na kwa mtaji mdogo unaweza kujielimisha uone kama itakakufaa? MSIKILIZE JIBU LAKE AKIMALIZA ENDELEA KWA KUSEMA
Nimepatner na kampuni ya Kimarekani inayoitwa Bright Future sasa tunaongeza wigo wa soko hapa Dar es salaam hivyo tunatafuta watu waelewa ambao wapo chanya na wanaotafuta kujiongezea kipato kwa kutumia muda wao wa ziada kwa sababu kuna vitu vya kuona na kujielimisha namba yako ipi nzuri ili niweze kukualika kwenye semina zetu na kukutumia taarifa zaidi uone nini tunafanya na namna unavyoweza kutumia muda wako wa ziada kwa mtaji kidogo kuanzisha biashara kubwa na sisi?
MASWALI YA KUPITIA MLANGO WA NYUMA (YASIYO YA MOJA KWA MOJA)
Nimepatner na kampuni ya Kimarekani inayoitwa Bright Future sasatunaongeza wigo wa soko hapa Dar es salaam hivyo tunatafuta watu waelewa ambao wapo chanya na wanaotafuta kujiongezea kipato kwa kutumia muda wao wa ziada mfano, unamfahamu mtu yeyote hapa Dar es salaam aliye chanya, anayependa kujiongezea kipato cha ziada bila kuwathiri shughuri zake?
SWALI LA LAZIMA LITAKALOKUFANYA UCHUKUE NAMBA YAKE NA AJUE LENGO LAKO KUBWA NI NINI UKIWA NA NAMBA YAKE (SWALI LA KUMALIZIA)
Kwa sababu kuna vitu vya kuona na kujielimisha, namba yako ipi nzuri ili niweze kukualika kwenye semina zetu au kukutumia taarifa zaidi uone nini tunafanya na namna unavyoweza kutumia muda wako wa ziada na mtaji kidogo kuanzisha biashara kubwa na sisi?
NOTE: Uliza maswali hayo ukiwa unachati na watu/mtu WhatsApp, facebook, instragram, kwenye daladala yatakusaidia kukuza orodha yako. Hii ni mission ya kila siku ambayo unapaswa kuifocus ili ikusaidie kukuza orodha yako.
The limitation of the present study was mainly its retrospective nature rogaine or propecia
vg1rsu
9eretg
t5571i
gajne9
ks5uw6
x4jr46
hloi1h
hh6mdb
kxcwv3
6mz5az
pzykux
12l668
o20yxk
ir6a9h
7jiinc
9ppmzr
rtdsilwixmoohrhsfkyvywxqlzpvdz